Tuesday, February 21, 2012

Keki Ya Nanasi



Vipimo: 
Unga                                                      2 vikombe vya chai 
Sukari                                                    1 ½ kikombe cha chai 
Mafuta                                                    1 ½ kikombe cha chai 
Baking powder                                         2 vijiko vya chai 
Siagi                                                       ¼ kikombe cha chai 
Mayai                                                      6 
Sukari ya hudhurungi (brown)                   1 ¾  kikombe cha chai 
Manasi ya kopo yaliyokatwa duara             1 kopo 
 
 
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika  
 
1.    Unayeyusha sukari ya hudhurungi  pamoja na siagi. Ikishayeyuka vizuri unamimina kwenye sufuria au trei ya kuchomea keki.
2.    Panga vipande  vya nanasi kwenye hiyo sufuria/trei. Weka pembeni. Ukipenda katikati ya duara ndogo ya nanasi weka cheri moja.
3.    Kwenye bakuli la kuchanganyia keki la mashine, piga mayai, sukari, vanilla mpaka iwe kamamalai (crème) na nzito.
4.    Mimina unga pamoja na baking powder, piga kidogo, mwisho mimina mafuta.
5.    Mimina huo mchanganyiko kwenye sufuria/trei uliyopanga vipande vya nanasi, tayari kuchoma.
6.    Weka moto 180 C choma kwa muda wa dakika 30 – 35.
7.    Ikishaiva, acha ipowe kwa muda wa dakika 7, mimina chini juu kwenya sahani, tayari kwa kuliwa.

No comments:

Post a Comment