Wednesday, February 29, 2012

Kamba Katika Sosi Ya Nazi


Vipimo

Kamba                                                           1 au 2 Pakiti
Chumvi                                                           Kiasi
Mafuta                                                           ¼ Kikombe
Bizari ya pilau (cummin) nzima                       ½ Kijiko cha chai
Vitungu                                                          2 Vikubwa
Nyanya zilioiiva                                              3
Nazi ya kopo au ya unga                                 2 Vijiko vya  supu
Siki au ndimu                                                 2 Vijiko vya supu
Pilipili  mbichi  iliyosagwa                                2 Vijiko vya chai
Vitungu vya kijani ( spring onions)                  3 Miche
  
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

   
1.     Osha kamba kwa maji ya baridi katika chungio, kisha weka  chumvi kiasi na iweke kwa firiji.
2.     Katika karai, weka mafuta yapate moto, tia bizari ya pilau lakini usiache ikaunguwa.
3.     Kisha tia vitungu na ukaange hadi zibadilike rangi ya hudhurungi lakini zisiungue.
4.     Halafu tia nyanya, tui la nazi , siki, pilipili na chumvi na iache motoni hadi nyanya zivurujike.
5.     Ongezea vitunguu vya kijani na ukoroge.
6.     Kisha tia kamba na uzipike hadi zibadilike rangi na kuiiva.
7.     Pakuwa na itakuwa tayari kwa kuliwa na wali au na mkate upendayo.

No comments:

Post a Comment